Victor Valdes azuiwa mazoezini Man United!!
Kwa mujibu wa ripoti inadaiwa kua mlinda mlango wa Man United,
Victor Valdes amekatazwa kuonekana eneo la mazoezi.
Gazeti la The Mirror limedai kua kocha Louis Van Gaal amemwambia kipa huyo kua anaweza kusogea eneo la mazoezi endapo tu kikosi cha kwanza hakipo mazoezini kwa hiyo anaweza kufanya mazoezi na makocha wa vijana.
Valdes mwenye miaka 33 amekua akihusishwa kutaka kuhamia vilabu vya Chelsea na Liverpool wiki iliyopita.
Kipa huyo wa zamani wa Barca alisaini United msimu uliopita kama chaguo la pili baada ya David De Gea ,lakini msimu huu amejikuta akiwa nyuma ya De Gea, Sergio Romero na Sam Johnstone.
Victor Valdes azuiwa mazoezini Man United!!
Reviewed by Steve
on
Tuesday, September 29, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Tuesday, September 29, 2015
Rating:

No comments:
Post a Comment