Arsenal waambulia sare na PSG, Wenger ametoa mtazamo wake
Matokeo: PSG 1-1 Arsenal
Tarehe: 13 September 2016
Uwanja: Parc des Princes
Arsene Wenger amewapongeza wachezaji wake kwa mchezo waliouonesha kupata pointi kwenye mechi ya klabu bingwa dhidi ya Paris-Saint Germain.
The Gunners walizidiwa kwa kiasi kikubwa lakini waliweza kujitetea kwa sare ya 1-1 ugenini, shukrani ziende kwa Alexis Sanchez kwa shambulizi alilofanya zikiwa zimesalia dakika 13 mchezo umalizike.
Edinson Cavani alifunga bao la kuongoza kwa wenyeji mapema kabisa, Wenger amekubali kwamba kikosi chake kilikosa kasi lakini walijitahidi na kuambulia pointi.
"Tulitaka kuanza kwa kasi kubwa lakini ndani ya dakika moja tukawa nyuma kwa 1-0. Ndani ya dakika 20 hatukuwa na kasi, walianza vizuri kuliko sisi lakini tulijikaza," aliwaambia waandishi "Tulicheza vizuri zaidi kipindi cha pili, wao walishuka kidogo.
Arsenal waambulia sare na PSG, Wenger ametoa mtazamo wake
Reviewed by Steve
on
Wednesday, September 14, 2016
Rating:
No comments:
Post a Comment