Propellerads

Haji Manara apata mwaliko wa kwenda akiwa mtupu jangwani!!, ona hapa



Msemaji wa Simba, Haji Manara amealikwa kesho kwenda kwenye
makao makuu ya klabu ya Yanga, eneo la mitaa ya Twiga na Jangwani akiwa mtu.

Msemaji wa Yanga, Jerry Muro amesema, Manara aende Jangwani akiwa mtupu kama alivyoahidi kama Simba ingepoteza mechi yake ya Jumamosi dhidi ya Yanga.

“Kweli ahadi ni deni, alisema atakuja akiwa mtupu kama Simba ingefungwa na Yanga. Sisi pia tungependa kumualika aje.

‘Napenda kumwambia Manara kwamba tumeishafanya usafi vizuri kabisa. Hivyo, akipenda anaweza kuja mapema kabisa ili kutimiza ahadi yake aliyokuwa ameitoa,” alisema Muro.

Simba ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-0 dhidi ya Yanga katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi.

Sasa Yanga inaongoza Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 12 sawa na Mtibwa Sugar na Azam FC, lakini zinatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa.

Lakini Manara alipoulizwa kuhusiana na hilo, alionyesha kushangazwa na kilichozungumzwa na Muro.

“Sijawahi hata siku moja kutoa ahadi hiyo, mara zote nimekuwa nikisistiza Simba itashinda na hilo ni jukumu langu kama kiongozi.


“Suala la kusema nitaenda nikiwa mtupu sijawahi kusema, pia nashangaa wakati ule Muro alisema atajiuzulu kama Yanga itafungwa na Simba. Tukawafunga lakini hakuna hata aliyemuuliza,” alisema Manara.
Haji Manara apata mwaliko wa kwenda akiwa mtupu jangwani!!, ona hapa Haji Manara apata mwaliko wa kwenda akiwa mtupu jangwani!!, ona hapa Reviewed by Steve on Monday, September 28, 2015 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.