Kama hukuisikia faini waliyolimwa Arsenal kutoka FA.
Club ya Arsenal imelimwa faini na chama cha soka cha Uingereza kutokana na tatizo lilitokea 26 July 2014. Kwenye
statement iliyotolewa na FA inasema kwamba “Arsenal wamekutwa na makosa ya kuvunja sheria za F.A kwenye mambo ya uwakala.”
“Makosa hayo yanatokana na uhamisho unamhusu Calum Chambers akiwa anatokea Southampton kwenda Arsenal July 26 mwaka 2014″
Uhamisho huo uliotumia £16 million imeripotiwa kwamba kulikua na uvunjwaji wa sheria za utaratibu hasa kwa upande wa uwakala. Baada ya maamuzi wakala Alan Middleton na club ya Arsenal wote wamelimwa faini isiyotajwa.
Calum Chambers amecheza mara 36 kwenye mashindano yote ya Arsenal tangu asajiliwe, tatizo hilo la faini halijamuathiri mchezaji na kazi yake.
Kama hukuisikia faini waliyolimwa Arsenal kutoka FA.
Reviewed by Steve
on
Saturday, June 13, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Saturday, June 13, 2015
Rating:
