Kiungo wa Yanga amsikitikia Boban.
Kiungo wa zamani wa Yanga, Akida Makunda, amebainisha kuwa iwapo
kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’
angezingatia nidhamu ya juu, angekuwa kuwa mchezaji wa
kipekee Simba ambaye angeheshimika na kustaafu soka kama Steven Gerrard wa Liverpool.
kipekee Simba ambaye angeheshimika na kustaafu soka kama Steven Gerrard wa Liverpool.
Makunda alisema: “Boban akiwa Simba alikuwa ni mchezaji bora,
aliheshimika sana lakini pia alikuwa ana jina kubwa, kitu pekee
kilichomtia doa ni ukosefu wa nidhamu ndani na nje ya uwanja.
“Naamini kama leo hii angezingatia nidhamu angemalizia soka lake
Simba na kuheshimika. Kwanza alikuwa ni mchezaji ambaye alijitoa kwa
Simba na hata hivyo naamini asingewahi kukubali kusajiliwa timu kama
Yanga kwasababu ya mapenzi aliyokuwa nayo kwa Simba.
“Boban angeweza kubaki na kuwa kama baba wa timu, nahodha na hata
kiranja mkuu kwenye timu hiyo lakini alipoteza bahati hiyo ambayo
ingeweza kumpa sifa ya kihistoria kwenye soka la Kitanzania.”
Mwaka 2013, Simba ilipokuwa ikinolewa na Kocha Mfaransa Patrick
Liewig, ilimsimamisha Boban na baadaye kuachana naye kutokana na kosa la
utovu wa nidhamu.
Baadaye
alijiunga Coastal Union ambayo aliichezea kwa msimu mmoja na kuachana
nayo. Hivi sasa ni mchezaji wa Friends Rangers ambayo inashiriki Ligi
Daraja la Kwanza.
Kiungo wa Yanga amsikitikia Boban.
Reviewed by Steve
on
Tuesday, May 26, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Tuesday, May 26, 2015
Rating:
