Neville: Liverpool imepoteza hadhi ya klabu kubwa
Nahodha wa zamani wa Manchester United, Garry Neville amesema
kauli ambayo huenda ikaendeleza ' bifu' lake na Liverpool baada ya
kusema
'mabingwa hao mara 18 wa zamani' wamepoteza hadhi ya klabu kubwa
na wanakaribia kuanguka kwenye kundi la timu ndogo.
"Kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita, mastaa wa Liverpool
wamekuwa waking'ang'ania kuondoka." anasema, Neville ambaye kwa sasa ni
kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya England, Three Lions. Liverpool
ilipoteza mchezo wa mwisho dhidi ya Stoke City baada ya kupokea kipigo
cha mabao 6-1, lakini Neville anachukulia kufeli kwa klabu hiyo ya
Mersyside kumsainisha mkataba mpya kiungo mshambulizi, Raheem Sterling
kama sababu ya Reds kuendelea kufanya vibaya."
"Kama utalinganisha na Manchester United kwa kipindi hicho,
utakuta mchezaji aliyeng'ang'ania kuondoka ni Cristiano Ronaldo."
aliongeza Neville, " Angalia Liverpool, iliwalazimu wawauze kwa
shingo-upande mastaa kama, Michael Owen, Steve McManaman, Luis Suarez na
wengineo."
"Anfield ni uwanja ambao una warudisha nyuma kwa sababu klabu
nyingine kubwa zimesonga mbele, kuongeza ukubwa wa uwanja au kujenga
uwanja mwingine."
Neville: Liverpool imepoteza hadhi ya klabu kubwa
Reviewed by Steve
on
Tuesday, May 26, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Tuesday, May 26, 2015
Rating:
