Propellerads

Drogba na sababu za kuondoka pia hatma yake baada ya Chelsea.


                                                      



Mshambuliaji wa  Chelsea Didier Drogba amethibitisha kua ataondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu, na amefafanua kua ni wapi anaelekea baada ya
Stamford Bridge.

 Drogba ambaye msimu huu amefanikiwa kuchukua taji la nne la Premier League akiwa na Chelsea, amedai kua bado anafikiria ni Ligi gani anaweza kwenda miongoni mwa ligi kubwa ulimwenguni.

Drogba aliulizwa kua kama anaweza kwenda ligi ya Marekani kama ikitokea akapata mkataba mnono huko.

"Ndio bila shaka, lakini nahitaji siku kadhaa, wiki kadhaa kufikiria kizuri zaidi kwangu hapo baadae. Kikubwanachotataka ni kucheza" Aliiambia ESPN.

Mkongwe huyo wa Chelsea amedai kukosa namba ya kudumu klabunindio sababu iliyomfanya aondoke, lakini anaamini kua kuna wachezaji vijana wengi ambao nao pia ni muda wao kung'aa.

"Niliongea na Jose (Mourinho) na bodi, na wote tukafikia mwafaka" Drogba aliongeza.

"Mwakani nataka nipate dakika zaidi kuliko nilizokua napata sasa. Nataka kucheza, labda naweza kumaliza niko juu"

"Kiukweli nahitaji kuendelea kucheza zaidi, kabla sijaacha soka napenda nifaidi kwanza kwa kupata muda wa kutosha uwanjani.

"Kwa hiyo mimi kuendelea kukaa halafu nimalize sina furaha, hiyo haitawezekana , kwa hiyo tulielewana na kukubaliana kipi chenye manufaa kwetu pande zote,

"Pia nadhani na timu inahitaji kua imara zaidi msimu ujao, kushindana klabu bingwa, na wananunua wachezaji wapya. Pia kuna chipukizi anbao nao wanahitaji kucheza

"Sio kwamba naogopa ushindani nao, ila naodhani ni muda wa kuwapa nafasi nao pia"

Drogba ameonekana katika michezo 28 akiwa Chelsea msimu huu, huku akicheza jumla ya dakika 869 pekee.
Drogba na sababu za kuondoka pia hatma yake baada ya Chelsea. Drogba na sababu za kuondoka pia hatma yake baada ya Chelsea. Reviewed by Steve on Wednesday, May 27, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.