Sababu tatu zinazoweza kumfanya Messi kuondoka Barcelona

Ripoti huko England zimemhusisha nyota wa FC Barcelona, Lionel Messi kutaka
kuhamia Manchester United na vilabu vingine (soma hapa)- hapa chini ni sababu tatu kwa nini anaweza kufanya hivyo, kiufupi kuondoka Catalan.
1) Pesa
Muarjentina anazidiwa kimapato na Ronaldo, ambapo bajeti ya mshahara Barcelona inaripotiwa kubanwa kiasi. Hata hivyo England timu kama United, pia Man City au Chelsea wanaweza kutenga pesa ndefu kumpata.
2) Mashitaka ya udanganyifu wa kodi
Messi anadaiwa kutokua na furaha kutokana na mashtaka ya sasa yanayomhusisha na kuchenga kodi Hispania. Wengi wanasema asingekua na matatizo kama haya England kwa sababu ya tofauti ya sheria katika mishahara ya wachezaji na haki ya jina.
3) Suala la kuthibitisha
Kumekuwepo na mijadala kua Messi hawezi kung'aa England. Ni kijana ambaye karibia maisha yake yote ya soka ametumikia Blaugrana, kwa hiyo endapo akihamia kwingine ni wakati wa kuthibitisha kwamba kweli yeye ndiye bora zaidi hata nje ya Barca.
Sababu tatu zinazoweza kumfanya Messi kuondoka Barcelona
Reviewed by Steve
on
Friday, October 23, 2015
Rating:



No comments:
Post a Comment