Yanga bado wanawafukuzia Simba
Yanga jana wamerejesha matumaini ya kuendelea na mbio za
kutetea ubingwa wao Tanzania bara baada ya kuwachapa Ruvu Shooting kwa mabao 2-0 uwanja wa Taifa jana.
Bao la kwanza la Yanga liliwekwa nayvuni na Simon Msuva dakika ya 31 kwa njia ya penalti, baada ya mwamuzi Ahmed Simba kuamuru ipigwe kufuatia beki wa Ruvu kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.
Emmanuel Martin aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Deus Kaseke, aliifungia Yanga bao la pili dakika za majeruhi kwa kichwa kumalizia krosi safi ya Msuva.
Yanga bado wanawafukuzia Simba
Reviewed by Steve
on
Thursday, March 02, 2017
Rating:
Reviewed by Steve
on
Thursday, March 02, 2017
Rating:

No comments:
Post a Comment