Propellerads

Mapato ya mechi ya watani Simba na Yanga yatangazwa, mgao utakua namna hii



Mechi ya ligi kuu bara iliyowakutanisha watani Simba na Yanga
Jumamosi iliyopita uwanja wa taifa Dar es Salaam, ulivuna kiasi cha shilingi milioni 324.

Akitangaza mapato hayo, Ofisa habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas, amesema mapato hayo yamepatikana baada ya kupiga hesabu za mashabiki waliojitokeza kutazama pambano hilo.

"Mechi ya Simba na Yanga imeingiza kiasi cha shilingi milioni mia tatu ishirini na nne laki moja na themanini, hiyo ni baada ya mashabiki wa pande zote kujitokeza kuliangalia pambano hilo ambalo lilikua na ushindani wa aina yake.

"Kwenye fedha hizo, Simba watapata asilimia 40 ( Sh milioni 129.6) ya fedha zote kwa sababu ya uenyeji wao, Yanga wakichukua asilimia 20 (Sh milioni 64.8) ya mapato yote kwa sababu wao walikuwa wageni wa pambano hilo.

"Lakini pia kuna taasisi ambazo zitachukua sehemu ya mapato hayo ambayo ni TFF asilimia 5, VAT asilimia 18, Selcom wao asilimia 5, Baraza la michezo Taifa (BMT) asilimia 1 na Chama Cha soka Dar es Salaa, (DRFA) asilimia 3.

"Nyingine ni gharama ya uwanja asilimia 15, Bodi ya Ligi (TPLB) wao asilimia 9, gharama ya mchezo mzima ulivyokuwa ikihusisha maandalizi asilimia 7."
Mapato ya mechi ya watani Simba na Yanga yatangazwa, mgao utakua namna hii Mapato ya mechi ya watani Simba na Yanga yatangazwa, mgao utakua namna hii Reviewed by Steve on Friday, March 03, 2017 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.