Propellerads

Tambwe akifunga leo, atavunja rekodi hizi





Endapo mshambuliaji wa Yanga, Amiss Tambwe, akifanikiwa kufunga katika

pambano la watani Simba vs Yanga, basi atakua amevunja rekodi za akina Kitwana Manara (Baba yake Haji Manara) na Madaraka Selemani.

Rekodi ambayo Tambwe ataivunja ni ya kufunga mara nne mfululizo katika mechi ya watani Simba na Yanga, mpaka sasa rekodi ipo hivi,

Kitwana Manara alipata kufunga mara tatu mfululizo

  • -March 30, 1968 Yanga 1-0 Sunderland
  • -Juni Mosi, 1968, Yanga 5-0 Sunderland
  • -Juni 04, 1972 ,Yanga 1-1 Simba

Madaraka Selemani

  • -Julai 2, 1994 ,Simba 4-1 Yanga
  • -Nov. 2, 1994, Simba 1-0 Yanga
  • -Nov. 21, 1994, Simba 2-0 Yanga

Tambwe yeye mpaka sasa yupo sawa na wakongwe hao, lakini endapo akifunga akifunga leo, basi atakua ameweka rekodi mpya, kwani kwa sasa hesabu zake zinasoma hivi;


  • -Septemba 26, 2015 (Simba 0-2 Yanga)
  • -Februari 20, 2016 (Yanga 0-2 Yanga)
  • Oktoba Mosi, 2016 Yanga 1-1 Simba



Tambwe akifunga leo, atavunja rekodi hizi Tambwe akifunga leo, atavunja rekodi hizi Reviewed by Steve on Saturday, February 25, 2017 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.