Stars walivyowanyonga Malawi leo uwanja wa Taifa
Taifa Stars imeanza vizuri kampeni ya kuwania kucheza Kombe
la Dunia baada ya kuitwanga Malawi kwa mabao 2-0.
Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Stars ilipata mabao yake yote mawili katika kipindi cha kwanza.
Bao la kwanza, lilitipiwa kimiani mapema tu na Mbwana Samatta ambaye alikuwa mwepesi kuiwahi pasi maridadi ya Thomas Ulimwengu na kufunga kwa ustadi mkubwa.
Ulimwengu, safari hii akipata ‘zawadi’ kutokana na kumfuatilia kipa wa Malawi aliyeutema mpira wa krosi wa Haji Mwinyi.
Hata hivyo, Malawi walionekana matata zaidi katika kipindi cha kwanza mwanzo wakitawala dakika zote 15 za mwanzo.
Kipindi Kocha Charles Boniface Mkwasa akiwa anaingoza Stars kwa mara ya kwanza akiwa Kocha Mkuu mwenye mkataba, aliwatoa Mrisho Ngassa akamuingiza Salum Telela na Simon Msuva akaingia badala ya Thomas Ulimwengu.
Mchezaji mwingine aliyeingia ni Ibrahim Ajibu na kufufua nguvu ya ushambuliaji ya Stars.
Hata hivyo, katika kipindi cha pili Stars walitoa nafasi nyingi zaidi kwa Malawi kushambulia zaidi.
Stars walivyowanyonga Malawi leo uwanja wa Taifa
Reviewed by Steve
on
Wednesday, October 07, 2015
Rating:
No comments:
Post a Comment