Propellerads

Hat trick aliyopiga Sanchez dhidi ya Leicester jana, Wenger amesema hivi




Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amempa sifa Alexis Sanchez
kwa kukubali kua nyota huyo anafaa kuitwa 'world class' baada ya kutupia hat trick jana dhidi ya Leicester.

Forward huyo kutoka Chile hakua amezifuma nyavu tangu Mei 4 walipoifunga Hull City 3-1. Lakini jana walipokutana na vijana wa Claudio Ranieri alitupia zake tatu zote kwa mashuti.

Wenger aliulizwa na Sky Sports kwamba Sanchez anaweza kuitwa 'world class'- neno ambalo limesikika sana wiki hii baada ya Sir Alex Ferguson kutaja wachezaji wanne wa aina hiyo aliopata kuwafundisha.

Wenger alijibu "Nadhani ni hivyo"

"Nadhani nina wachezaji wengi ambao ni world class. Unatakiwa uelewe maana ya hii lakini yote kwa yote  (Sanchez) ni mshambuliaji mwenye hamasa na anayejituma kwa ajili ya timu. Kama timu ikicheza vizuri anaweza kufunga magoli."

Magoli mengine ya Arsenal yalifungwa na Walcott na Giroud hivyo kuipa Arsenal matokeo ya 5-2 mbele ya Leicester ambao magoli yao nao yalifungwa na Vardy na Drinkwater.

Pia katika mechi nyingine EPL zilizochezwa jana matokeo yalikua hivi

Spurs 4-1 Man City

Leicester 2-5 Arsenal

Liverpool  3-2 Aston Villa

Man Utd 3-0 Sunderland

Southampton 3-1 Swansea

Stoke 2-1 Bournemouth

West Ham 2-2 Norwich

Newcastle 2-2 Chelsea




Hat trick aliyopiga Sanchez dhidi ya Leicester jana, Wenger amesema hivi Hat trick aliyopiga Sanchez dhidi ya Leicester jana, Wenger amesema hivi Reviewed by Steve on Sunday, September 27, 2015 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.