Mourinho ataja nyota asiotaka kuwapoteza.
Bosi wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amedai kua itakua ngumu kwake kuendelea kukaa na
nyota wote ikiwemo Eden Hazard na Cesc Fabregas.
Mourinho amesema kua malengo yake ni kutowauza baadhi ya nyota, ambapo amewataja baadhi.
"Katika misimu mingine, nilikua naweza kuuza baadhi ya wachezaji hata waliokua ni wakali" aliiambia Mirror.
"Lakini msimu huu siwezi kuwauza wachezaji wangu wazuri, kwa hiyo changamoto kubwa ni kuendelea nao.
"Kama nikiendelea na Eden Hazard, Nemanja Matic, Branislav Ivanovic, Diego Costa na Cesc Fabregas, hilo ni lengom langu kubwa."
Kocha huyo akiwa na Chelsea amechukua ubingwa wa EPL mara tatu, kombe la FA mara moja, na kombe la ligi mara tatu.
Mourinho ataja nyota asiotaka kuwapoteza.
Reviewed by Steve
on
Wednesday, June 10, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Wednesday, June 10, 2015
Rating:
