Ronaldo awapa hofu Real Madrid, kisa hiki hapa
Akimaliza msimu wa 2014/2015 bila kombe,
Ronaldo anaamini kuna utofauti mkubwa kati ya mafanikio ya ufungaji wa
magoli aliyopata Real Madrid na idadi ya makombe aliyoshindaa
havilingani. Kiufupi Ronaldo anaumizwa na ukame wa makombe katika klabu
ya Real Madrid.
Gazeti la Marca leo limechapisha habari
mbaya kwa mashabiki wa Real Madrid , likileta hofu kwamba siku si nyingi
Cristiano Ronaldo anaweza kuondoka Los Blancos
Kwa namna Marca walivyoeleza katika stori
hiyo, Cristiano Ronaldo anajiona kuwa mtu rahisi Santiago Bernabeu na
ana wasiwasi kutokana na muelekea wa sasa wa klabu.
Pia Ronaldo bado ana kinyongo, Marca
limesema kwamba mshindi huyo wa Ballon d’Or amechukizwa na Real Madrid
kushindwa kumsapoti kuelekea katika sherehe yake ya kuzaliwa akitimiza
miaka 30.
Yote kwa yote, Ronaldo anahitaji ‘Mpango
wa Ushindi’ Real Madrid, wakati matajiri wa Ufaransa wanasikilizia kama
nyota huyo wa kimataifa wa Ureno ataonesha nia ya kuondoka Real Madrid.
Tazama ukurasa wa mbele wa gazeti la Maca leo ukija na stori hiyo :
Ronaldo awapa hofu Real Madrid, kisa hiki hapa
Reviewed by Steve
on
Thursday, May 21, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Thursday, May 21, 2015
Rating:

