Messi na mkataba wa Simba
Uongozi wa Klabu ya Simba umemtega kiungo wake
mshambuliaji, Ramadhan Singano ‘Messi’ kwa kumtaka atafakari kwa mara nyingine
kuhusu dau la shilingi milioni 30 alilotajiwa, badala ya shilingi
milioni 50 anazotaka.
milioni 50 anazotaka.
Singano ambaye alipandishwa kutoka kikosi cha
Simba B, inaelezwa kuwa anatembea na mkataba aliopewa kwa kuwa anahitaji
kutafakari kabla ya kusaini.
"Tumempa
mkataba, alisema anataka kuwapa watu wake wa karibu wauangalie na
kumshauri, hivyo tumempa afanye hivyo," alisema Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe.
![]() |
| Ramadhan Singano "Messi" |
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba uongozi wa Simba umekuwa katika mikakati ya kuachana na wachezaji wote wanaousumbua.
Hivyo
kama Messi ataendelea kuusumbua kwa madai ya kuongezewa dau kubwa zaidi
kwa kuwa tu Jonas Mkude alilipwa dau kubwa, basi utaachana naye na
kuangalia njia nyingine.
Messi na mkataba wa Simba
Reviewed by Steve
on
Friday, May 22, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Friday, May 22, 2015
Rating:
