Propellerads

Ibe, Flanagan kuendelea Liverpool

Jordon Ibe akisaini mkataba mpya na klabu yake ya Liverpool ambao utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka
2020
Winga  wa Liverpool Jordon Ibe na beki Jon Flanagan wamesaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu yao.
Ibe, ambaye hapo awali alikuwa akikipiga kwa mkopo katika klabu ya Derby, amedondoka saini ya miaka mitano ambayo imemuongezea maslahi zaidi kuliko alipokuwa akikipiga katika ‘academy’ ya klabu hiyo.
Flanagan ambaye amekuwa ametoka kufanyiwa upasuaji wa pili wa goti, amesaini mkataba wa mwaka mmoja ambao utamuwezesha kubaki klabuni hapo mpaka mwakani




Baada ya kusaini mkataba huo mpya Ibe alisema,”Nilifurahi sana mara baada ya kuitwa kwenye timu hii ya wakubwa, na nimefurahi pia kupewa nafasi ya kuitumikia klabu yangu. Natumaini nitaendelea kutoa mchango mkubwa sana kadiri muda unavyokwenda.”
Ibe, Flanagan kuendelea Liverpool Ibe, Flanagan kuendelea Liverpool Reviewed by Steve on Saturday, May 23, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.