Hatimaye Yanga yamng'oa huyu
![]() |
| Kaseke |
Kiungo nyota aliyetamba na Mbeya City, Deus Kaseke sasa ni mali ya Yanga.
Mabingwa hao walikuwa wakipambana kuimarisha kikosi chao kwa ajili ya michuano ya kimataifa.
KAseke amejiunga na Yanga baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili, jana.
Taarifa kutoka ndani ya Yanga zimeeleza, Kaseke amemaliza na uongozi wa Yanga jana, hivyo sasa ni mali ya Jangwani.
Kabla ya hapo, kulikuwa na taarifa za kiungo huyo kuwaniwa na Yanga na Azam FC.
Simba walikuwa wa kwanza kutaka kumsajili msimu uliopita, lakini zoezi hilo likakwama.
Meneja wake, naye alilizungumzia msimu huu baada ya kusema walikuwa wakizungumza na Yanga na walifikia hatua nzuri zaidi.
Hatimaye Yanga yamng'oa huyu
Reviewed by Steve
on
Monday, May 25, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Monday, May 25, 2015
Rating:
