Propellerads

Deco ataja wachezaji wawili ambao alikua hapendi kukutana nao


Deco akipambanana Scholes


Mchezaji wa zamani wa vilabu vya Chelsea na Barcelona, Deco de Souza ametaja wachezaji ambao walikua wakimpa upinzani mkali mpaka kufikia yeye kutopenda
kupambana nao

Mchezaji huyo mstaafu wa kimataifa kutoka Ureno amewamwagia sifa mkongwe wa Ma U Paul Scholes na pia bosi wa Atletico madrid , Diego Simeone kua ni wachezaji waliokua wakimpa wakati mgumu sana.

"Paul Scholes alikua ni miongoni mwa viungo bora katika historia" Aliiambia Four Four Two.

"Haijawahi kutokea kwa timu kubwa, hajapata kufunga magoli mengi, lakini aliipangilia timu vizuri sana.

"Ninapoangalia mechi,hua nawaangalia sana viungo, wanawarahisishia washambuliaji.

"Scholes na Diego Simeone walikua mwiba kwangu"

Akivichezea vilabu vya FC Porto, Barcelona, Chelsea na Fluminense ya Brazil, kiungo huyo amepata kufunga mabao 39 katika mechi 350 alizocheza, huku akitoa usaidizi mara 66.

Pia ameichezea timu yake ya taifa ya Ureno mechi 75, ni miongoni mwa wachezaji wachache kupata kuchukua kombe la UEFA mara mbili katika vilabu viwili  tofaut,i FC Porto na Barcelona.
Deco ataja wachezaji wawili ambao alikua hapendi kukutana nao Deco ataja wachezaji wawili ambao alikua hapendi kukutana nao Reviewed by Steve on Saturday, May 23, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.