Cristiano Ronaldo aweka wazi umri atakaostaafu soka
Alhamisi hii Ronaldo alishinda tuzo ya mchezaji bora Ulaya ya UEFA ya 2016 baada ya kuisaidia Real Madrid kuchukua taji la Ulaya mara ya 11 huku pia akiiongoza Ureno kushinda taji la Euro mwaka 2016.
Ronaldo ameuita mwaka 2016 kama "usiosahaulika kwa klabu na nchi" na amekanusha madai kua anaingia hatua ya mwishoni katika wakati wake kwenye soka kwani anajiandaa kumalizia soka lake Santiago Bernabeu.
"Ulikua ni mwaka usiosahaulika kwa klabu na nchi, ilikua vizuri na nina furaha . [UEFA Best Player] ni taji muhimu sana, na baada ya kushinda makombe mawili makubwa zaidi kwa klabu na timu ya taifa, kushinda taji hili ni swala la kukumbuka sana huu mwaka." Ronaldo aliwaambia waandishi.
"Nipo katika klabu bora ulimwenguni na ninataka kustaafia hapa, nikifikisha 41, na kama nilivyosema kabla lengo langu ni kuongeza mkataba na kukaa."
Cristiano Ronaldo aweka wazi umri atakaostaafu soka
Reviewed by Steve
on
Saturday, August 27, 2016
Rating:
Reviewed by Steve
on
Saturday, August 27, 2016
Rating:




No comments:
Post a Comment