Propellerads

Matola amepiga chini Simba, hizi hapa ni sababu kadhaa


                         

Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola ameamua kubwaga manyanga na
kuachana na kazi yake hiyo.
Matola, nahodha wa zamani wa Simba, alifanya kikao cha saa zima na Rais wa Simba, Evans Aveva lakini akashikilia msimamo wake.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Simba zinaeleza mambo haya matatu yalichangia Matola kuachana na Simba.

Moja:
Hawakuwa wakielewana na Kocha Dylan Kerr katika masuala mengi, jhambo ambalo Matola aliona kwake lisingekuwa jambo zuri na mwisho angeangushiwa mzigo.

Pili:
Matola alidai Kerr hakuwa akipokea ushauri wake wa aina yoyote, lakini akafikia hatua ya kupanga kikosi bila ya kumshirikisha. Wakati mwingine Matola aliijua timu mbele ya wachezaji wakati wakitangaziwa.

Tatu:
Matola alianza kuchukizwa kuona Kerr akifanya kikao na wachezaji huku akimtoa yeye pamoja na staff wengine wa benchi la ufundi, jambo pia aliona si sahihi.

Nne:
Kocha huyo mzalendo, anamshutumu Kerr kumchonganisha na wachezaji akitaka yeye kuonekana ni mbaya.

Tano:
Matola anaamini urafiki wake wa kikazi na Kerr ulianza kuzorota baada ya yeye kushikilia msimamo wa kutaka kocha Mserbia wa viungo abaki kwa kuwa Simba inamhitaji lakini taarifa zinaeleza tayari uhusiano wa Mserbia yule na Kerr ulishavurugika kabisa ndiyo maana wakati anaondoka alisema lazima Simba itafungwa na Yanga, kweli ikafungwa.

Matola amepiga chini Simba, hizi hapa ni sababu kadhaa Matola amepiga chini Simba, hizi hapa ni sababu kadhaa Reviewed by Steve on Thursday, November 12, 2015 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.