Van Gaal: De Gea hachezi tena mechi ijayo
Kipa ambae anatakiwa kwa hamu kubwa na Real Madrid bado ataendelea
kukaa benchi kwenye mechi dhibi ya Aston Villa kama ilivyokua kwenye mechi ya ufunguzi.
Licha ya De Gea kusema kwamba yupo tayari kucheza kwa sasa lakini kocha Van Gaal amesema kwamba hapana De Gea hatacheza kwenye mechi ijayo dhidi ya Aston Villa. Akielezea kwanini De Gea ata miss hiyo safari ni kutokana na kwamba bado yupo kwenye hali ile ile iliyosababisha kukosa namba mechi ya kwanza.
Sababu aliyoitoa kwa De Gea kukosa nafasi kwenye mechi ya ufunguzi ilikua ni kwasababu ya kua kwenye hali mbaya kisaikolojia kwasababu ya mambo ya uhamisho. De Gea anahusishwa sana na kuhama club ya Manchester, hili swala halimuweki vizuri kisaikoloji hivyo basi sio rahisi kucheza vizuri. Kwasababu kipindi cha usajili bado kipo, basi bado yupo kwenye hilo tatizo ndio maana hatacheza kwenye hii mechi pia.
Van Gaal: De Gea hachezi tena mechi ijayo
Reviewed by Steve
on
Friday, August 14, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Friday, August 14, 2015
Rating:




No comments:
Post a Comment