Uganda wamaliza ukame wa miaka 38 kucheza AFCON, pia kuna matokeo mengine na timu zote zilizofuzu
Uganda 1-0 Comoros
Uganda wamefuzu kucheza michuano ya kombe la mataifa Afrika kwa mara ya kwanza
ndani ya miaka 37, baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Comoro, shukrani zimwendee mshambuliaji Farouk Miya.
Burkina Faso 2-1 Botswana
Burkina Faso nao wamejichukulia tiketi yao kuelekea Gabon, baada ya kushinda kwa 2-1 mbele ya Botswana katika kundi D.
Malawi 1-0 Swaziland
Goli la Gerard Phiri Jr dakika ya 8 lilitosha kuwapatia ushindi wa kuongoza Malawi katika mchezo wao wa mwisho kundi L, hata hivyo timu hizi zote hajijafuzu kucheza Afcon.
Guinea 1-0 Zimbabwe
Zimbabwe wao walimaliza kwa kipigo kutoka kwa Guinea, lakini hata hivyo wao tayari walishafuzu.
Tunisia 4-1 Liberia
Katika kundi A, Tunisia wamefuzu kwa kuwachapa Liberia kwa mabao 4-1.
Togo 5-0 Djibouti
Togo wamefuzu wakiwa ni miongoni mwa vikosi bora kabisa baada ya kuwachapa Togo kwa 5-0 katika mchezo uliopigwa Jumapili jioni.
Algeria 6-0 Lesotho
Algeria wamemaliza mbio za kuelekea Afcon kwa ushindi mkubwa wa 6-0 mbele ya Lesotho Jumapili jioni kwa mabao ya Riyad Mahrez, El Arbu Soudani, Saphir Taider na Ryad Boudebouz.
Timu 16 zilizofuzu: Gabon, Cameroon, Algeria, Zimbabwe, Tunisia, Togo, DRC, Mali, Burkina Faso, Uganda, Guinea-Bissau, Morocco, Egypt, Ghana, Ivory Coast, Senegal.
Uganda wamaliza ukame wa miaka 38 kucheza AFCON, pia kuna matokeo mengine na timu zote zilizofuzu
Reviewed by Steve
on
Monday, September 05, 2016
Rating:
Reviewed by Steve
on
Monday, September 05, 2016
Rating:

No comments:
Post a Comment