Kumbe mzungu wa Simba anakunwa sana na Tambwe, soma hapa!!
Straika wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe,
amezua balaa jipya katika Klabu ya Simba baada ya kocha mkuu wa timu hiyo,
Muingereza, Dylan Kerr, kuhoji kwa nini aliondoka klabuni hapo.
Kerr alifikia hatua hiyo baada ya
kumshuhudia Tambwe katika luninga akiiongoza Yanga kuibuka na ushindi wa mabao
2-0 katika mchezo wake wa ufunguzi wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union ya jijini
Tanga.
Kiongozi
mmoja wa juu wa Simba ambaye aliomba kutotajwa jina lake, alisema Kerr baada ya
kumshuhudia Tambwe akiwatengenezea wachezaji wenzake nafasi hizo za mabao,
alihoji na kutaka kujua sababu iliyoifanya Simba iachane naye.
“Nilipomwambia sababu yenyewe alisikitika
sana kwani alidai kuwa tulimuacha mchezaji mzuri ambaye kama msimu huu
angekuwepo kikosini, basi angekuwa na msaada mkubwa sana katika kikosi chake.
Hata hivyo, Kerr alipoulizwa kuhusiana na
jinsi alivyomuona Tambwe katika mchezo huo, alisema: “Ni mchezaji mzuri lakini
kwa sasa siwezi kumzungumzia kwa sababu hayupo kwenye kikosi changu.”
Kumbe mzungu wa Simba anakunwa sana na Tambwe, soma hapa!!
Reviewed by Steve
on
Wednesday, September 16, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Wednesday, September 16, 2015
Rating:

No comments:
Post a Comment