Propellerads

Umeisikia hii ya kocha wa Simba kuwataka Samatta na Ulimwengu!!

                                


Inawezekana ikawashtua mashabiki na wadau wa Simba
lakini habari ni kuwa, kocha mkuu wa timu hiyo, Dylan Kerr, amewataja washambuliaji wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu kuwa ni aina ya wachezaji ambao anawahitaji kikosini kwake.

Kerr amesema kama ikitokea wachezaji hao wakamaliza mikataba yao kwenye klabu yao ya sasa, basi anatamani kuona wanatua Simba na ikiwa hivyo basi mambo yatakuwa bambam kwake katika idara ya ushambuliaji.

Kauli hiyo inaweza kushangaza wengi kwa kuwa inajulikana wachezaji hao kwa sasa mipango yao ni kwenda nje ya Afrika kucheza soka la kulipwa na siyo kurejea Tanzania kucheza katika ngazi ya klabu.

Kerr alitamka hivyo juzi mara baada ya kuwaona Samatta na Ulimwengu wakiiongoza Taifa Stars kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Malawi, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Akizungumza na Championi Ijumaa, Kerr alisema amevutiwa na viwango vilivyoonyeshwa na washambuliaji hao aliowapa sifa ya upambanaji licha ya kudai pia walipoteza nafasi nyingi za kufunga.

“Kwenye mechi ya Stars nimefurahishwa na viwango vya wachezaji wote, lakini sana ni wale washambuliaji wawili, yule aliyevaa jezi namba 10 (Samatta), namba 11 (Ulimwengu) na Ndemla (Said).

“Hao ni aina ya wachezaji ninaowahitaji kwenye kikosi changu kutokana na uwezo wa kupambana na kuwasumbua mabeki.

“Ninaamini kama nikiwapata kwenye kikosi changu, basi nitafurahi nikiamini kuwa tatizo la umaliziaji litakuwa limemalizika kutokana na uwezo wa washambuliaji hao,” alisema Kerr.

Hata kabla ya msimu kuanza, Simba ilikuwa bize ikitafuta mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao mengi, licha ya Kerr kuletewa wachezaji kadhaa, bado ilionekana hakuna ambaye amekidhi vigezo, ndipo hatua ya mwisho wakasajiliwa Msenegal, Pape Nd’aw, Mussa Mgosi na Mganda, Hamis Kiiza.
Umeisikia hii ya kocha wa Simba kuwataka Samatta na Ulimwengu!! Umeisikia hii ya kocha wa Simba kuwataka Samatta na Ulimwengu!! Reviewed by Steve on Friday, October 09, 2015 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.