Mabeki hata wakimkamia Ngoma ataendelea kutupia tu
Baada ya kufunga bao lake la kwanza la Ligi Kuu Bara ikiwa
ndiyo mechi yake ya kwanza ya ligi hiyo, Donald Ngoma amesema ataendelea kuifungia Yanga.
Ngoma raia wa Zimbabwe amesema ana imani kubwa ya kuendelea kufanya vizuri kutokana na ushirikiano wa kikosi hicho.
“Ninajua mabeki watanipania sana, watataka kunizuia lakini ndiyo kazi yao. Mimi nitakachofanya ni kufunga kila nitakapopata nafasi,” alisema.
Ngoma alifunga bao la pili wakati Yanga ikiididimiza Coastal Union kwa mabao 2-0.
Straika huyo aliyejiunga na Yanga msimu huu akitokea FC Platnum ya Zimbabwe alionekana kuandamwa na ukame wa mabao wakati wa mechi za kirafiki zikiwemo zile za Kombe la Kagame ambazo Yanga iliishia robo fain
Mabeki hata wakimkamia Ngoma ataendelea kutupia tu
Reviewed by Steve
on
Tuesday, September 15, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Tuesday, September 15, 2015
Rating:

No comments:
Post a Comment