Propellerads

Unamkumbuka kocha Razack Siwa aliyekua Yanga!!...atua klabu hii




Aliyewahi kuwa kocha wa makipa wa Yanga na Coastal Union, Mkenya, Razack Siwa, amefanikiwa kujiunga na Klabu ya African Sports kwa mwaka mmoja akiungana na kocha mkuu mpya Mrage Kabange aliyetokea Kagera Sugar.


Siwa amekwisha zimetumikia klabu kadhaa hapa nchini ikiwemo Yanga katika msimu  wa 2013/14 na kutimkia Coastal  msimu uliopita ambako hakudumu kutokana na kushindwana kimaslahi.

Meneja wa timu hiyo, Ahmed Boznia, alisema lengo la kuwa na makocha hao ni kuhakikisha wanakuwa imara msimu ujao kutokana na kuwa na uzoefu kwenye ligi hiyo.

 “Razack Siwa tumeingia naye mkataba wa mwaka mmoja, ataungana na kocha Mrage Kabange ambaye naye tayari tumemalizana kwa mwaka mmoja, hivyo tuna nguvu ya kutosha kuelekea msimu ujao kuweza kukabiliana na ushindani.


“Lakini pia baada ya kumsajili Nsa Job, pia  tumefanikiwa kumnasa beki wa kati wa zamani wa Simba, Rahim Juma Abdallah, hivyo tumejiimarisha,”a lisema Boznia.
Unamkumbuka kocha Razack Siwa aliyekua Yanga!!...atua klabu hii Unamkumbuka kocha Razack Siwa aliyekua Yanga!!...atua klabu hii Reviewed by Steve on Wednesday, July 01, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.