Yanga wampa baraka zote Mkwasa.
Hatimaye Yanga imekubali kumuachia Kocha wake msaidizi Charles Boniface Mkwasa ainoe Taifa Stars.
Hata hivyo imeelezwa Mkwasa akisaidiana na Mohammed Morocco atakuwa ni kocha wa muda tu.
Awali Yanga ilikuwa imeweka ngumu, hata hivyo baadaye imekubali baada ya uongozi wa TFF kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji.
Taarifa zinaeleza, itamtambulisha Mkwasa leo asubuhi kwenye mkutano mbele ya waandishi.
Morocco ambaye pia alikuwa wa kwanza kukubali wito, pia atatambulishwa hii leo.
Yanga wampa baraka zote Mkwasa.
Reviewed by Steve
on
Tuesday, June 23, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Tuesday, June 23, 2015
Rating:
