Di Maria alivyopamba headlines Ufaransa
Gazeti la kila siku la Ufaransa la L’Equipe leo limebeba Headline ya stori inayowagusa mashabiki wa Manchester United.
Kwa mujibu wa ripoti, muda wa
Angel di Maria kukaa Man United unaelekea kufikia tamati ambapo PSG
wanataka kumsajili nyota huyo wa Argentina majira ya kiangazi mwaka huu.
L’Equipe wanaripoti kwamba PSG wanahitaji mshambuliaji anayetokea pembeni, hivyo wanaamini Di Maria anafaa kabisa.
Sehemu ya stori inayovutia ni
kwamba PSG wanaweza kujaribu kumujumuisha katika dili hilo beki wao wa
Kulia, Mholanzi, Gregory Van der Wiel.
Inaaminika kuwa Man United wanahitaji beki wa kulia majira ya kiangazi na Vander Wiel anaweza kuwashawishi kumuuza Di Maria kwa PSG.
Di Maria alivyopamba headlines Ufaransa
Reviewed by Steve
on
Monday, May 25, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Monday, May 25, 2015
Rating:
