Cheki mkwara wa Vidal kwa Arsenal

Artulo Vidal amewapiga mkwara Arsenal kua watarajie kukutana
na Bayern Munich 'yenyewe' ambapo wakali hao wa Bavaria wanajipanga kulipa kipigo cha klabu bingwa wiki mbili zilizopita.
The Gunners waliwafunga 2-0 vijana wa Pep Guardiola na kujiokoa kutoka mstari wa hatari katika kundi F baada ya kupoteza michezo miwili ya mwanzo.
Wakali hao watakutana tena Allianz Arena Jumatano hii, lakini kiungo huyo wa Chile amedai itakua ni habari nyingine.
"Tutawaonesha Arsenal Jumatano Bayern Munich ya ukweli" aliiambia Bild "Confidence yetu ni kubwa. Safari hii tutatumia nafasi zetu na tutachukua point tatu."
Cheki mkwara wa Vidal kwa Arsenal
Reviewed by Steve
on
Monday, November 02, 2015
Rating:

No comments:
Post a Comment