Propellerads

Kopunovic asema Simba wakimpata huyu atawasaidia sana......soma hapa kujua ni nani

 
 
 
Kocha wa zamani wa Simba, Goran Kopunovic amesema iwapo Simba watafanikiwa kumnasa Laudit Mavugo, atatoa msaada mkubwa katika safu ya ushambuliaji.

Akizungumza na mtandao mmoja, Kopunovic amesema Mavugo ni mmoja wa wachezaji wenye kiwango kizuri katika ushambuliaji.

“Ni mshambuliaji mzuri, ana kasi, nguvu, anapiga mashuti, pia mzuri wa mipira ya juu kutokana na mfumo unaotumiwa na kocha.


“Ninaamini ataongeza chachu ya Simba kuwa na safu nzuri ya ushambuliaji,” alisema Kopunovic ambaye ndiye alimpendekeza Mavugo raia wa Burundi.

Mavugo sasa ni mshambuliaji tegemeo wa Vital’O ya Burundi. Pia timu ya taifa ya Burundi na tayari yuko katika hatua nzuri ya mazungumzo na mshambuliaji huyo.


Kabla Mavugo aliwahi kufanya kazi pamoja na Kopunovic katika kikosi cha Polisi Rwanda.



Kopunovic asema Simba wakimpata huyu atawasaidia sana......soma hapa kujua ni nani Kopunovic asema Simba wakimpata huyu atawasaidia sana......soma hapa kujua ni nani Reviewed by Steve on Sunday, May 31, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.