Orodha ya wachezaji 'world class' kwa Ferguson, Rio Ferdinand ameiongelea hivi
Rio Ferdinand ameibuka baada ya Sir Alex Ferguson kutomweka
kwenye orodha ya wachezaji wenye hadhi ya 'world class' aliopata kuwafundisha.
Katika kitabu chake cha sasa kiitwacho 'Leading' kocha huyo mskochi ameandika majina manne ya wachezaji ambao aliwafundisha na ambao kweli ni nyota wa kiwango cha juu au kwa maana nyingine world class amabpo amewataja Cristiano Ronaldo, Paul Scholes, Ryan Giggs na Eric Cantona.
Na Rio Ferdinand anaonekana kushangazwa kwanini jina lake halimo kwenye orodha hiyo ya wakali wa Man United, hali iliyopelekea yeye kuja na swali kua "World class ni nini?"
"Nini kinafanya mtu anakua world class?" Ferdinand aliandika Facebook "Sir Alex Ferguson ametaja majina manne kwa wakati wake akiwa MUFC kua ndio World Class (Jina langu lilikua wapi kati ya majina machache bosi!!)
Mwisho kabisa Ferdinand alionekana kuonesha kua sasa kuna kile kinachoonekana kua kama mabishano kuhusu majina hayo miongoni mwa mashabiki wengi kwa sasa.
Orodha ya wachezaji 'world class' kwa Ferguson, Rio Ferdinand ameiongelea hivi
Reviewed by Steve
on
Thursday, September 24, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Thursday, September 24, 2015
Rating:




No comments:
Post a Comment