Kumbe Pele anafagilia zaidi The Gunners, amesema haya
Nguli wa soka ulimwenguni, Pele amesema kama angepata fursa
ya kucheza ligi kuu nchini Uingereza, basi angekipiga kunako klabu ya Arsenal.
Pele amedai kuwa mtindo wanaocheza Barcelona unafafana sana timu yake ya zamani ya Santos, ambayo aliichezea kati ya mwaka 1956 na 1974.
Alipoulizwa ni timu gani angependa kucheza nchini Uingereza, Pele alijibu.
“Arsenal ingekuwa ndio sehemu pekee ambayo ningeweza kucheza”, Pele aliliambia gazeti la Telegraph .
“Napenda sana timu ambazo hucheza mchezo wa kujiachia/kufunguka uwanjani. Kwa sasa ni vigumu mno kusema ni timu gani ambayo inacheza mchezo huo.
Kumbe Pele anafagilia zaidi The Gunners, amesema haya
Reviewed by Steve
on
Saturday, September 26, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Saturday, September 26, 2015
Rating:




No comments:
Post a Comment