Propellerads

Gareth Bale azungumzia uhusiano wake na Ronaldo klabuni Real Madrid, je ni kweli hawaelewani?



Nyota wa Real Madrid, Gareth Bale amefichua ukweli kuhusu
uhusiano wake na mchezaji mwenzie klabuni hapo, Cristiano Ronaldo.

Bale ameweka hali ilivyo kati yake na Ronaldo ambapo watu wengi walikua wakiamini kua wachezaji hao hazipikiki haziivi pamoja.

Tofauti na imani hiyo ya watu wengi, Bale amesema Ronaldo amekua kama muongozo wake klabuni hapo

"Kujifunza kutoka kwa mchezaji bora zaidi duniani ni kitu kikubwa sana" aliiambia WalesOnline.

"Ananikosha sana tangu niwasili hapa na nimekua najifunza vitu vipya kila siku.

"Ananisaidia sana mimi kuja kua mchezaji bora zaidi duniani, kitu ambacho ni lengo langu kubwa."

Pia Bale alisema anatarajia kufikia mafanikio ambayo Ronaldo anayo.

"Najitahidi kufikia level kama yake.

""Naangali mbele zaidi na kujua nini nitafanya" alimaliza Bale

Bale aliyejiunga Los Blancos mwaka 2013 akitokea Tottenham, amefunga magoli 39 na kutoa usaidizi mara 31 katika michezo 93 Santiago Bernabou.



Gareth Bale azungumzia uhusiano wake na Ronaldo klabuni Real Madrid, je ni kweli hawaelewani? Gareth Bale azungumzia uhusiano wake na Ronaldo klabuni Real Madrid, je ni kweli hawaelewani? Reviewed by Steve on Friday, August 28, 2015 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.