Van Persie anataka kiasi hiki kutoka kwa Man United.
Nyota Robin van Persie ameripotiwa kudai alipwe kiasi cha
pauni mil 12 ili aweze kuondoka klabuni hapo.
Mchezaji huyo mwenye miaka 31 amekua akihusishwa sana na kutaka kuondoka klabuni, inadaiwa tayari ameshafanya makubaliano na klabu a Fenerbahce ya Uturuki.
United wanajiandaa kumruhusu Mdachi huyo aondoke kwa kumlipa kiasi cha pauni mil 5 ili kufidia kiasi cha 250, 000 anacholipwa kwa wiki, huku waturuki nao wanataka kumpa thamani hiyo hiyo aliyoipata Man U.
Hata hivyo, van Persie anataka alipwe gharama zake za mshahara za mwaka wake wa mwisho klabuni hapo ambazo zinafikia kiasi cha pauni mil 12 kabla hajaondoka Old Traford, The mirror wameripoti.
Bestikas na Galatasaray pia wanahusishwa kutaka kumnasa mshambuliaji huyo.
Van Persie anataka kiasi hiki kutoka kwa Man United.
Reviewed by Steve
on
Sunday, July 05, 2015
Rating:
Reviewed by Steve
on
Sunday, July 05, 2015
Rating:



