Wenger anahofia kumkosa kiungo wake huyu kutokana na majeraha
Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger ameonesha wasiwasi wake
kumkosa kiungo mkabaji Francis Coquelin kwa muda mrefu kidogo.
Mfaransa huyo aliumia kwenye mechi waliyoshinda kwa 3-0 mbele ya Chelsea Jumamosi, sasa meneja wake anahofia yasije kutokea ya msimu uliopita ambapo Coquelin alikaa nje miezi miwili kutokana na majeraha.
"Ana jeraha kwenye goti na alikua hivyo tena mwaka jana alipokua West Brom," Wenger alisema kama alivyonukuliwa na The Independent, "Hiyo ni mbaya ya siku.
"Hatujajua kama jeraha ni kubwa lakini ngoja tusubiri. Lakini kuondoka uwanjani amefungwa inanipa wasiwasi."
Wenger anahofia kumkosa kiungo wake huyu kutokana na majeraha
Reviewed by Steve
on
Monday, September 26, 2016
Rating:
Reviewed by Steve
on
Monday, September 26, 2016
Rating:


No comments:
Post a Comment