Propellerads

Barcelona na Neymar kuchunguzwa tena




Uhamisho wa nyota Mbrazil Neymar kujiunga na Barcelona unatarajiwa kuchunguzwa tena, mara hii ukifanywa na La Liga.

Uhalali wa mchezaji huyo kuhama mwaka 2013 kuja Barca akitokea Santos ya Brazil umekua katika utata mwingi tangu awasili.

Inaaminika ada ya uhamisho iliyotangazwa haikua sahihi na sasa La Liga wamethibitisha kwamba watafanya uchunguzi wao huku kesi ya kwanza ikiwa imeshasikilizwa ambapo klabu hiyo ya Catalunya ikikiri makosa.

"Kufuatia kuenea habari mbali mbali, La Liga imethibitisha kua uchunguzi utafanyika kwa Barcelona kuhusu makubaliano yaliyofikiwa kati ya ofisi ya mwendesha mashitaka na bodi ya klabu kuhusu kesi ya Neymar" tangazo rasmi lililotolewa na La Liga.

Rais wa Barca, Josep Maria Bartomeu mapema mwaka huu alikubali kulipa faini ambayo ilionesha klabu hiyo kukiri makosa, lakini ni bado kidogo kesi hiyo kumalizika kabisa.


Barcelona na Neymar kuchunguzwa tena Barcelona na Neymar kuchunguzwa tena Reviewed by Steve on Friday, September 16, 2016 Rating: 5

No comments:

Propellerads
Powered by Blogger.