Propellerads

Baada ya Gerard kuondoka, Xavi Hernandez nae.

Wakati dunia ikijadili  kama maamuzi ya Steven Gerrard kwenda La Galaxy ya Marekani ni sahihi, baba mzazi wa Xavi Hernandez, Joaquim Hernandez amesema
mwanae ataondoka Barcelona kwenda kumalizia soka lake katika klabu ya Al Sadd ya Quatar.
Xavi ambaye amecheza Barcelona tangu akiwa mtoto kwa miaka ya karibuni hana namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza, lakini ni miongoni mwa mashujaa wa kikosi cha Hispania waliotwaa ubingwa kombe la mataifa ya Ulaya na dunia.

Xavi


Baba mzazi wa Xaiv amesema tayari maamuzi yameshafikiwa na kilichobaki ni mwanae kuaga, huku akifichua kuwa katika mkataba anaotarajia kusaini Al Sadd unamruhusu kuwa kocha mchezaji.
Hata hivyo taarifa za ndani kutoka Barcelona zinasema kiungo huyo mkongwe atafanya mkutano wa kuaga na waandishi wa habari alhamisi ya juma hili.
Mkataba wa Xavi na mabingwa hao wapya wa Hispania unamalizika mwakani, lakini ameamua kuondoka zake baada ya msimu huu kumalizika.
Baada ya Gerard kuondoka, Xavi Hernandez nae. Baada ya Gerard kuondoka, Xavi Hernandez nae. Reviewed by Steve on Tuesday, May 19, 2015 Rating: 5
Propellerads
Powered by Blogger.