Hatma ya mikataba ya Sanchez na Ozil klabuni Arsenal
Arsenal wana imani kubwa kuendelea kuwa na nyota wawili
Mesut Ozil na Alexis Sanchez katika mikataba ya muda mrefu hivyo kuzima tetesi zote kuhusu hatma yao.
Wawili hao kila mmoja amebakiza miaka miwili katika mkataba wa sasa, lakini kwa mujibu wa The Mirror, watendaji klabuni Arsenal wana mpango wa kuwashawishi nyota hao kusaini tena, huku kwa upande wa Ozil ikionekana kuwasili kwa Shkodran Mustafi ambaye ni swahiba yake ni sababu inayoweza kumshawishi zaidi.
Sanchez alihusishwa sana kutaka kuhamia Juventus huku Ozil yeye Real Madrid wakitaka kumchukua tena.
Hatma ya mikataba ya Sanchez na Ozil klabuni Arsenal
Reviewed by Steve
on
Monday, September 12, 2016
Rating:
Reviewed by Steve
on
Monday, September 12, 2016
Rating:

No comments:
Post a Comment