Baada ya kuzinguana na Guardiola, Yaya Toure afunguka ukweli wake kwa mara ya kwanza
Mchezaji bora Afrika mara nne, Yaya Toure amevunja ukimya wake
tangu atolewe katika kikosi cha UEFA klabuni Manchester City na kocha Pep Gaurdiola.
Kapteni huyo mstaafu wa Ivory Coast bado anafanya mazoezi na kikosi cha kwanza Man City japokua Guardiola alitoa kauli kwamba hatompanga tena mpaka wakala wake atakapoomba radhi kwa maoni yake kwenye vyombo vya habari.
Baada ya kipindi cha mazoezi jana Jumanne, Toure alifunguka kupitia mtandao wa Twitter kwamba ni ngumu kwake.
"Kipindi kizuri cha mazoezi asubuhi hii. Vigumu kutocheza klabu bingwa. Lakini nadhani wenzangu wapo vizuri kwa kesho (leo)." ali tweet.
Kwa mujibu wa ESPN, nyota huyo alikua na furaha kipindi cha mazoezi ambapo vyombo vya habari vilipewa nafasi kwa dakika 15 za mwanzo pekee.Good training session this morning. Difficult not being involved in Champions League, but I wish my team mates good luck for tomorrow! 🙌🏾 pic.twitter.com/9YgAqVU1h8— Yaya Touré (@YayaToure) September 27, 2016
Baada ya kuzinguana na Guardiola, Yaya Toure afunguka ukweli wake kwa mara ya kwanza
Reviewed by Steve
on
Wednesday, September 28, 2016
Rating:

No comments:
Post a Comment